Dar es salaam Police Academy

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Camillus Wambura, tarehe 31 Januari 2024 amefunga rasmi Mahafali ya Saba na Nane ya Vyuo vya Polisi katika fani mbalimbali za kitaaluma ikiwemo Stashahada na Astashahada ya upelelzi wa Makosa ya Jinai, Sayansi ya Polisi, Usalama Majini na Mawasiliano ya Polisi ambapo zaidi ya wahitimu 897 walitunukiwa katika mahafali hayo yaliyofanyika kwenye viwanja vya Chuo cha Taaluma ya Polisi Kurasini jijini Dar es salaam.